Halloween party ideas 2015

Sheria ni nini?
Sheria ni masharti yanayowekwa katika nchi ili kutoa mwongozo wa jinsi ya kufanya mambo kwa usahihi. Sheria lazima zifuatwe na watu wote, na anayevunja sheria huadhibiwa.
Kanuni ni nini?
Kanuni ni maagizo kwa ajili ya asasi kubwa ya umma, zinazoongoza kufanya mambo yaliyo sahihi. Kanuni hizi mara nyingi zinafafanua sheria za nchi.
Taratibu ni nini?
Taratibu ni maelekezo yanayotolewa kwa idara zote za serikali ili kuelekeza kufanya mambo yaliyo sahihi.
1. Mwalimu ni nani katika mazingira yetu ya Tanzania?
Neno “mwalimu” limetafsiriwa kwenye ‘Kamusi ya Kiswahili Sanifu’ TUKI (1981) kwenye ukurasa wa 201 kuwa ni “mtu afundishaye elimu au maarifa Fulani, au mtu anayeonesha wengine”.
Katika Sheria ya Elimu, (sura ya 353 R.E.2002), neon ‘mwalimu’ limepewa maana kwenye fungu la 2 (1) kuwa ni “mtu yeyote aliyesajiliwa kama mwalimu chini ya sheria hii.”
Na fungu la (46) la sheria hii, linaonesha kuwa baada ya mtu kusajiliwa na Kamishna wa Elimu na kupewa cheti, basi mtu huyo anakuwa mwalimu.
2. Umuhimu wa mwalimu kufahamu sheria
Ili mwalimu aweze kutekeleza kwa ufanisi wajibu wake mbele ya umma anapaswa awe na sheria na miongozo ambayo itamsaidia kuelewa vyema utumishi wake kama mtumishi wa umma.
Kanuni za Mpango wa Utumishi wa Umma za mwaka 2005, zilizotolewa kwenye Gazeti la Serikali namba 331 la tarehe 28/10/2005 ambazo zinahusu watumishi wa umma wakiwemo na walimu zinaonesha nyaraka za sheria ambazo mtumishi wa umma anapaswa kuwa nazo.
Kanuni ya 31 (1) ya kanuni hizo inaorodhesha nyaraka hizo kuwa ni;
  1.  Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, (sura ya 2 R.E. 2002)
  2. Sheria ya Utumishi wa Umma (sura ya 298 R.E. 2002)
  3. Sheria ya Huduma ya Mafao ya Kustaafu (sura ya 371 R.E. 2002
  4. Sheria ya Mafao ya Kustaafu ya Viongozi wa Kisiasa (sura ya 225 R.E.2002)
  5. Sheria ya Huduma ya Umma (chombo cha upatanishi)
  6. Sheria ya Uajiri na Uhusiano wa Kazi (sura ya 366)
  7. Sheria ya Wakala wa Serikali (sura ya 245 R.E. 2002)
  8. Sheria ya Utawala wa Mkoa (sura ya 97 R.E. 2002)
  9. Sheria ya Taasisi za Kazi (sura ya 300)
  10. Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2003
  11. Kanuni za Maadili na Tabia za Watumishi wa umma,
  12.  Kanuni mbalimbali za maadili na mwenendo wa wataalam
  13. Kanuni za Serikali kwa ajili ya huduma za Umma
  14. Kanuni za kuajiri wahudumu wa umma
  15. Kanuni za nidhamu ya wahudumu wa umma
  16. Kanuni ya usuluhishi na mapatano ya huduma ya umma
  17. Kanuni za kustaafu na kuachishwa kazi ya huduma ya umma
  18. Kanuni ya sera ya uongozi na uajiri wa huduma ya umma
  19. Sheria nyingine za nyaraka zinazohusika kwa ajili ya marejeo yanayohusika
3. Je, mtumishi wa kawaida anaweza kuzipata wapi hizi sheria na nyaraka anazopaswa kuwa nazo mtumishi wa umma?
Kwa mujibu wa kanuni ya 31 (2) na (3) ya Kanuni za Mpango wa Utumishi wa Umma za mwaka 2005 zinaeleza kuwa, “Kila mwajiri atapaswa kuhakikisha upatikanaji na fursa ya kutumia nyaraka zote anazopaswa kuwa nazo mtumishi aliye chini yake”.
SIKU hizi haipiti dakika hujasikia haki zikidaiwa mahali. Kuna haki za watoto. Haki za akina mama. Haki za wafanyakazi wa ndani(Koero analizungumzia hili vizuri). Haki za masikini. Haki za vyangudoa. Haki za maalbino. Haki za wasomaji. Haki za mafisadi (hata fisadi naye ana haki ya kusikilizwa/natural justice). Haki. Haki. Haki. Orodha ni ndefu.

Jambo moja. Inapodaiwa haki, ikumbukwe kuwa upo upande ambao utalazimika kunyang'anywa haki zake ili haki ile ya kwanza inayodaiwa ipatikane. Kwa maneno mengine, unajikuta ili kutetea haki, inabidi unyang'anye haki. Na upande huu wa pili unaolazimika kupoteza haki ili kufidia haki inayodaiwa, nao ukiamka, inabidi zoezi liwe mduara. Yaani poteza haki, kuleta haki.

Kwa mfano. Mtoto anapodai haki, maana yake inamlazimu mzazi kupoteza haki zake ili kumpatia mwanae haki. Kwa maneno mengine, haki ya mtoto inakuwa utumwa kwa mzazi. Unapoteza haki kuleta haki.

Mwanafunzi wa kike anapodai haki ya kusoma kwa upendeleo, inabidi mamlaka zinazohusika kubinya haki za wavulana ili haki hiyo inayodaiwa itimie. Hapa, maana yake unapoteza haki ili kuleta haki.

Sasa hapa ndiko liliko swali langu: Haki ni nini?

Na haki hizi ni kwa ajili ya nani, jamii, kikundi cha watu fulani wanaodai rehema ama ni mtu binafsi?

Inakuwaje kama tukiamua kuzivunja haki hizi? Je, haki ni kutii sheria na taratibu zilizopo kwa lengo tu la kuepuka adhabu?

Je, haki ni kile kinachoweza kufanywa na watu wengine ili kutupa faida hata kama kufanya hivyo kunawaumiza wao? (Je, wao hawana haki?)

Je, haki ni kuwa mtu mzuri anayekubalika kwenye jamii? (Vipi kama nikiamua kutafuta haki zangu kwa namna ninayoijua mimi hata kama kwa kufanya hivyo ntaonekana kituko?)

Je, haki ni kutimiza matakwa ya sheria zilizopo hata kama zinaingilia uhuru wangu?

Je, haki ni kutetea matakwa ya wengine, hata kama kufanya hivyo kunakunyima vitu fulani fulani
Je, haki ni matakwa ya kibinafsi yasilazimika kushahibiana na sheria zinazoonekna ni halali katika jamii?

Kumbuka palipo na haki kuna haramu. Pasipo tafsiri nzuri ya haki, tunajikuta kila tunalolifanya ni haramu. Mzunguko wa madai usioisha. Kupoteza haki. Kupata haki. Kupoteza tena. Kuzipata tena. Mwishowe, kila kitu kinakuwa haramu

Post a Comment

Powered by Blogger.